Wednesday, August 15, 2012

PRECISION AIR NA TAASISI YA TUMAINI LA MAISHA KUTOA USAFIRI KWA WATOTO WENYE SARATANI


 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Precision Air Bw. Alfonse Kioko akizungumza na wageni na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kutiliana saini na Taasisi binafsi ya Tumaini la Maisha ambapo amesema kuwa taifa lenye afya ndio lenye uwezo wa kupata maendeleo na kuongeza kuwa watoto wanahitaji uangalizi na huduma bora za afya ili kujenga taifa lenye afya bora na mafanikio siku za usoni. Kushoto ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Tumaini la Maisha Bi. Blandina Lugendo na kulia ni Daktari Bingwa wa Saratani za Watoto (Paediatric Oncologist) Dkt. Trish Scalan. 



Bw. Alfonse Kioko wa Precision air wakitiliana saini mkataba na Bi. Blandina Lugendo wa Taasisi ya Tumaini la Maisha, utakaoshuhudia kampuni ya Precision Air ikitoa tiketi za ndege kwa Taasisi ya Tumaini la Maisha Tanzania, ambazo zitatumika kusafirisha watoto wenye saratani pamoja na wazazi au walezi wao kutoka jijini Dar es Salaam kwenda sehemu mbalimbali nchini.



Wakikabidhiana mkataba wa makubaliano hayo.


Kampuni ya huduma za usafirishaji wa anga ya Precision Air imeingia katika ubia na taasisi binafsi ya Tumaini la Maisha Tanzania ambayo inajihusisha na kuboresha maisha ya watoto wenye saratani nchini Tanzania.

Kampuni hiyo itakuwa ikitoa tiketi mbili zilizolipiwa ushuru kwa mwezi na kuwezesha kusafirisha wagonjwa kwenda katika maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza katika hafla ya kusain imkataba wa ubiahuo, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Precision Air Bw. Alfonse Kioko amesema wanayo furaha kuingia katika ushirikiano huo katika jitihada za kujenga taifa lenye afya.

Bw. Kioko ameongoza kusema kuwa wapo maelfu ya watoto wanaosumbuliwa na saratani ndani ya nchi yetu, na ni lengo lao sasa kuhakikisha tunawarahisishia ugumu wa maisha katika kupambana na ugonjwa huo.

Taasisi ya Tumaini la Maisha Tanzania imekuwa taasisi ya kwanza  ya kijamii yenye dhamira ya kuboresha afya za watoto waishio na ugonjwa wa saratani nchini Tanzania.
Moja ya malengo ya Taasisi hiyo ni pamoja na kujenga wodi mpya ya Saratani katika hospitali ya taifa Muhimbili ili kuweza kutoa huduma kwa watoto na familia zao na kuepuka wingi wa wagonjwa katika wodi za hospitali hiyo.

SOURCE: www.dewjiblog.com
 ________________ 
Media Contact:
E-mail: thpi2009@gmail.com



No comments:

Post a Comment