Tuesday, May 15, 2012

WAHITIMU VYUO VIKUU TUMIENI TAALUMA YENU KUTENGENEZA AJIRA




Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Dk. Mary Nagu (MB) amewataka wahitimu wa vyuo vikuu katika fani mbalimbali hapa nchini kutumia elimu na utaalamu wanaoupata katika vyuo  mbalimbali hapa nchini  kwa kuweka mipango madhubuti ya kujiajiri.

Nagu aliyasema hayo wakati alipoongoza  matembezi ya “SAIDIA  MAMA MJAMZITO KUJIFUNGUA SALAMA” yaliyoandaliwa na Taasisi ya Madaktari wahitimu wa Vyuo Vikuu Tanzania (THPI) yaliyoanzia katika hospitali ya Manispaa ya Temeke mpaka Ofisi za Manisipaa ya hiyo, Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Februari 2012.

“Kwa niaba ya serikali napenda kuwapongeza Taasisi ya Madaktari Wahitimu wa Vyuo Vikuu Tanzania kwa kuwa chachu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika  kuwezesha vijana kujiajiri na napenda kuwahakikishia kuwa serikali inatambua mchango wenu wa kuunga mkono serikali katika kuboresha huduma za afya kwa akina mama na watoto” alisema Nagu

Aliongeza kuwa maendeleo ya elimu  nchini ya mechochea kuongezeka kwa vyuo vikuu hapa nchini na idadi ya wahitimu katika vyuo hivyo , ikiwa ni ishara ya uthubutu na utayari wa serikali katika kuwekeza na kusimamia sekta ya elimu hapa nchini lakini bado idadi ndogo ya wahitimu wanaoweza kupata ajira  katika sekta ya umma na binafsi kutokana na ufinyu wa nafasi hizo.

Aidha  Nagu alifafanua kuwa pamoja na kuwa Taasisi hiyo kuwa  inatengeneza ajira kwa vijana jambo kubwa  inalolitekeleza vizuri ni kwa kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha afya ya Mama mjamzito hapa nchini ,mpango wenye lengo la kupunguza  vifo kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga.

Awali akimkaribisha Nagu, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Madaktari Wahitimu Vyuo vikuu Tanzania,  Dk. Telesphory Kyaruzi alieleza kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni jinsi ya kuwapelekea huduma wanachi kwa wakati na kwa gharama wanazoweza kuzimudu.

Dr. Kyaruzi albainisha kuwa ukubwa wa changamoto huo pia unatokana na jinsi ya kuwafikia wananchi na hasa akina mama.

Katika mwaka 2010 kumekuwa na mafanikio makubwa katika kupungua kwa vifo vya mama wajawazito na wototo kufikia 454 kati ya watoto hai 100,000 kutoka 578 kwa mwaka 2005.



Friday, May 4, 2012

DKT. JAKAYA KIKWETE ATANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI



Mh. Dr. Fenella E. Mukangara (MB) (Katikati) atangazwa kuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

MAWAZIRI

1. OFISI YA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,

2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H.  Suluhu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

3.  OFISI  YA WAZIRI MKUU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

4.  WIZARA

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,
Waziri wa Ujenzi
Dr.  John P. Magufuli, Mb.,
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,
Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,
Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof.  Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof.  Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,
Waziri wa  Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,
Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,

Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,
Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,
Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,
Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,

5. NAIBU MAWAZIRI

OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI

6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

7.OFISI YA WAZIRI MKUU

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,

8. WIZARA MBALIMBALI

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,
Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,
Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,
Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
4 Mei, 2012

Saturday, April 14, 2012

MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA KAMPENI YA KITAIFA YA UHAMASISHAJI WA UCHANGIAJI DAMU KUOKOA MAISHA YA MAMA WAJAWAZITO WANAOHITAJI DAMU.


Dkt. Telesphory Tryphone Kyaruzi Mkurugenzi Mtendaji wa THPI akipeana mikono na Mgeni Rasmi Mama Salma Kikwete Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) mara baada ya kutoa hotuba yake ya utangulizi. Katikati ni Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh. Dkt. Fenella Mukangara (MB).



Katika hotuba yake ya utangulizi Dkt. Telesphory Kyaruzi, alianza kwa kumshukuru Mgeni Rasmi Mama Sama Kikwete kwa kukubali kuwa Mgeni Rasmi katika kampeni hii ya Kitaifa ya kuchangia damu. Alisema kampeni kuu ya Saidia Mama Mjamzito ajifungue Salama inalenga kuhamasisha Taifa juu ya kutekeleza malengo ya milenia namba 4 na 5 ya kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa asilimia 75 ifikapo mwaka 2015. Alisema swala lakuchangia damu ni swala ambalo liko katika uwezo wetu sisi watanzania. Alisema pia kwamba hiyo ni awamu ya kwanza ya kampeni hiyo ambayo kampeni itaendelea mikoani ikiwamo Shinyanga, Kigoma, Mbeya na hatimaye Tanzania nzima.



Nae Naibu Waziri Wizara Ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dkt. Fenella Mukangara (MB), alimshukuru Mama Salma Kikwete na kumpongez a kwa kujali changamoto zinazowakabili wakina Mama na Watoto na kushiriki katika kutatua changamoto hizo. Pia aliwashukuru na kuwapongeza madaktari Vijana kupitia umoja wao wa THPI kwa kubuni na kuanzisha kampeni hiyo. Pia wizara yake ambayo ina dhamana na mambo ya Vijana, imechukulia hatua hiyo ni muendelezo wa sera ya Maendeleo ya vijana ya mwaka 2007 ambayo inaendelea kutumika hadi sasa. Pia alisema kwamba Wizara inawahimiza kuendelea kuthubutu na kupenda kazi na kujituma kwa kuzingatia sheria na malengo chanya ya kujenga Taifa letu la Tanzania. Wizara inahimiza Vijana kutumia fursa kwa kutumia weledi na utaalam wao katika Maendeleo ya Taifa. Amefurahishwa sana jinsi Vijana madaktari wameweza kutumia utaalam wao kwa kutatua kero ambayo wamekutana nayo katika sehemu yao ya kazi. Aliendelea kusema kwamba mpango unalenga katika kuhamasisha Taifa kuchangia damu ili kuweza kumaliza vifo vya kina mama na watoto. Alichukua fursa hiyo kuwataka Vijana walio kaitka taaluma mbali mbali (Youth Profesionals) kote nchini Tanzania kuweza kujiunga katika kutoa huduma mbali mbali kwa jamii kulingana na taaluma zao.



Nae Mgeni rasmi Mama Salma Kikwete katika hotuba yake alianza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana katika uzinduzi wa Kitaifa wa kampeni ya kuchangia damu, shughuli ambayo ni muhimu kwa ustawi wa Taifa letu la Tanzania. Pia aliendelea kwa kuwapongeza madaktari Vijana wa THPI kwa kusema kwamba jambo waliliolifanya ni kubwa sana Kitaifa, la kukusanya damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya kina mama na watoto wanaohitaji damu. Aliwataka madaktari Vijana wa THPI kuendelea kuwa na moyo huo huo bila kujali changa moto zinazowakabili, na aliahidi kuendelea kuwaunga mkono katika jitihada zao kadri muda utakavyo mruhusu. Mama Salma Kikwete alisema kuwa ifikapo mwaka 2015 lazima tuhakikishe kwamba tumefikia malengo ya MDG 4 na 5 ya kuboresha Afya ya Mtoto na kupunguza vifo vya kina mama. Alisema Tanzania imepiga hatua kubwa kwa kupunguza vifo vya watoto kutoka 578 kati ya vizazi hai 100,000 mpaka kufikia 454 kati ya vizazi hai 100,000 kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na taasisi mbali mbali ikiwemo THPI. Alisema kwamba ifikapo mwaka 2015 Tanzania itafikia malengo ya milenia kwa kupunguza vifo vya kina mama na watoto mpaka kufikia 225 kwa vizazi hai 100,000. Alimaliza kwa kuwataka Vijana wote wa Tanzania kuonyesha moyo wa uzalendo kwa Taifa letu. Pia alitoa shukurani zake za dhati kwa ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji chini ya Mh. Dkt. Mary Nagu (MB), kwa Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Mh. Dkt. Fenella E. Mukangara (MB), na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii chini ya Dkt. Hadji Mponda (MB) kwa kuwawezesha Vijana madaktari kutekeleza shughuli mbali mbali ikiwemo kampeni hii. Pia Aliwapongeza wakina mama na kina baba na wananchi wote waliohudhuria katika kampeni hiyo wakiwemo wanafunzi wa Shule za Sekondari mbali mbali.



“VIJANA TUSONGE MBELEE, HATUWEZI KURUDI NYUMAA * 2,
SONGAA, SONGA MBELEE, HATUWEZI KURUDII NYUMA * 2”



Katibu Mkuu Wa THPI Dkt. Elisia Mpango katika kutoa shukrani kwa niaba ya THPI kwenye kuhitimisha kampeni hiyo alitoa shukrani zake za dhati kwa Mgeni rasmi mama Salma Kikwete kwa kukubali kushirki na kuzindua rasmi kampeni hiyo, pia alitoa shukrani kwa Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (MB) , Mstahiki Meya wa Kinondoni Mh. Yusuph Mwenda, Katibu Tawala za Mikoa Mh. Bi. Theresia Mbando, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii iliyowakilishwa na Dkt. Donan Mbando na wadau wote walioshiriki katika kukamilisha kampeni hiyo bila kuwasahau wakina mama, wakina baba, Vijana na wanafunzi wa sekondari na wote walioshiriki na kukubali kuchangia damu kwa hiari yao. Alisema katika kampeni hiyo jumla ya chupa 150 za damu zilikusanywa. Aliwaasa wahisani mbali mbali wajitokeze katika awamu zinazofuata za kampeni hiyo ili kuwezesha mwendelezo wa kampeni ya SAIDIA MAMA MJAMZITO AJIFUNGUE SALAMA.




Friday, April 6, 2012

THPI YAANZISHA KAMPENI YA KITAIFA YA KUCHANGIA DAMU ILIYOZINDULIWA NA MAMA SALMA KIKWETE


Mkurugenzi mtendaji wa THPI Dr. Telesphory Kyaruzi akitoa historia fupi ya taasisi hiyo pamoja na kuelezea kampeni ya "Saidia mama mjamzito ajifungue salama" kwa kuchangia damu katika awamu ya kwanza kitaifa. Wanaofuatilia kulia ni Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh. Dkt. Fenella E. Mukangara (MB), mgeni rasmi Mama Salma Kikwete mwenyekiti wa taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) , na katibu tawala mkoa wa Dar es Salaam Bi. Theresia Mbando.
Kampeni imelenga kukusanya damu kwa ajili ya kuwasaidia wakina mama wajawazito wanaohitaji damu kabla ya kujifungua wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua, na wale ambao wanajifungua kwa upasuaji.

Monday, April 2, 2012

THPI YAANDAA KAMPENI YA KITAIFA YA KUCHANGISHA DAMU ILIYOZINDULIWA NA MAMA SALMA KIKWETE




Mama Salma Kikwete akiwasili katika viwanja vya Biafra Kinondoni wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kuchangisha damu iliyofanyika katika viwanja hivyo. Anaesalimiana nae ni naibu waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo Mh. Dkt. Fenella Mukangara (MB) na anaefuata ni meya wa kinondoni Mh. Yusuph Mwenda. Katika kampeni hiyo jumla ya unit 150 za damu zilipatikana na zitatumika kuwasaidia wakina mama wajawazito wanaohitaji damu.

Friday, March 30, 2012

PRESS RELEASE

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KAMPENI YA KUCHANGISHA DAMU KUSAIDIA MAMA WAJAWAZITO WENYE UPUNGUFU WA DAMU WAJIFUNGUE SALAMA, AWAMU YA KWANZA

Taasisi ya madaktari wahitimu vyuo vikuu vya Tanzania, Tanzania Health Promotion Initiative (THPI) kwa heshima na taadhima wanayo furaha kubwa kuujulisha umma wa Tanzania kwamba tarehe 31/03/2012 Jumamosi kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 7 mchana tutaendesha zoezi la kuhamasisha taifa kuchangia damu.

Lengo ni kuhamasisha wa Tanzania kujenga utaratibu wa kwenda kuchangia damu mara kwa mara kadiri inavyoshauriwa ili kuwa na damu ya kutosha katika vituo vyetu. Ikiwa ni jitihada ya kuokoa maisha wakina mama wajawazito wanaopata matatizo ya upungufu wa damu wakati wa ujauzito, kabla ya kujifungua na baada ya kujifungua.

Kuna upungufu mkubwa wa damu katika hospitali zetu hivyo wananchi tujenge tabia ya kuchangia damu ili kuondoa tatizo hili.

Huu ni mwendelezo wa kampeni yetu kuu ya “Saidia mama mjamzito ajifungue salama” ambayo ni kampeni ya kitaifa inayolenga kuhamasisha taifa kutekeleza malengo ya millennia lengo la 4 na la 5 ya kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Mama Salma Kikwete, Mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na maendeleo.

Shukrani kwa Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara kwa kusaidia kufanikisha maandalizi ya kampeni hii.
Tunashukuru taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) kwa kutupa ushirikiano madaktari vijana katika kampeni hii.

Wito kwa serikali iendelee kushirikiana na wadau mbali mbali ili kuongeza ufanisi katika kupunza vifo vya mama na watoto. Kwa vyombo vya habari kusaidia kuelimisha na kuhamasisha umma kujielekeza kusaidia mama wajawazito wajifungue salama. Kwa wananchi tunaomba muitikio wao katika kuchangia damu ili kusaidia mama wajawazito wenye upungufu wa damu. Tunatoa rai kwa wahisani kuongeza nguvu ya kifedha kufanikisha kampeni hii.

Imetolewa na:

Dkt. Elisia Mpango

Katibu Mkuu

Tanzania Health Promotion Initiative - THPI

Tuesday, March 27, 2012

KAMPENI YA KITAIFA JUU YA UHAMASISHAJI WA UCHANGIAJI DAMU KUOKOA MAISHA YA MAMA WAJAWAZITO WANAOHITAJI DAMU.

THPI
TANZANIA HEALTH PROMOTION INITIATIVE
( Taasisi ya Madaktari Wahitimu Vyuo Vikuu Vya Tanzania)


Kwa Kushirikiana na

Kitengo Cha Damu Salama Cha Taifa na Kitengo Cha Damu Salama Kanda ya Pwani.


KAMPENI YA KITAIFA JUU YA UHAMASISHAJI WA UCHANGIAJI DAMU KUOKOA MAISHA YA MAMA WAJAWAZITO WANAOHITAJI DAMU, AWAMU YA KWANZA.


Kauli Mbiu: Jiwekee Utaratibu wa Kuchangia Damu, Okoa Maisha ya Mama Mjamzito

Lengo: Kukusanya Damu kwa ajili ya Kusaidia mama wajawazito Hospitali za Temeke,
Amana, Mwananyamala na Muhimbili.

Kampeni Kuu: Saidia Mama Mjamzito Ajifungue Salama.


Mahali: Viwanja Vya Biafra, Kinondoni Dar es Salaam.

Muda: Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 7:00 Mchana

Tarehe: Jumamosi Tarehe 31/03/2012

Mgeni Rasmi: Mama Salma Kikwete- Mwenyekiti Taasisi ya Wanawake na Maendeleo- WAMA.

Utangulizi.

Kuelekea mwaka 2015, nchi nyingi Duniani zinaelekeza jitihada na nguvu zao katika kufika malengo ya milenia, hasa lengo la 4 na 5, kupunguza vifo vya mama na motto. Ni nchi 21 Duniani zilizo katika mwelekeo sahihi wa kufikia malengo ya millennia kuelekea mwaka 2015.

Takribani wakinamama 368,000 duniani wanapoteza maisha kutokana na ujauzito. Taarifa za dunia zinaonyesha kuwa wakina mama wajawazito walio katika nchi zenye idadi kubwa ya vifo vya mama na mtoto wako katika hatari ya kupoteza maisha mara 100 zaidi kulinganisha na nchi ambapo idadi ya vifo vya mama na mtoto ni ndogo.

Kwa upande wa Tanzania vifo vya mama na mtoto vimepungua kutoka 578/100000 kwa mwaka 2005 hadi 454/100000 kwa takwimu za mwaka 2010. Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa upande wa Tanzania UNDP-Tanzania linasema pamoja na kushuka kwa idadi ya vifo, bado changamoto ni kubwa sana.

Wakina mama wengi wajawazito wanapoteza maisha kutokana na kukosa damu, wengine wanamatatizo ya kupoteza damu wakati wa ujauzito (anaemia in pregnancy) kabla ya kujifungua(Ante-partum haemorrhage), baada ya kujifungua (Post-partum haemorrhage). Mara nyingi maabara zetu hazina damu za kutosha kila wakati kusaidia mama wajawazito wenye matatizo ya damu, mara nyingi wanapelekwa hospitali za rufaa na wengi wanakufa njiani.

Hivyo basi Taasisi ya Madaktari Wahitimu Vyuo Vikuu Vya Tanzania, Tanzania Health Promotion Initiative, THPI, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali itaendesha kampeni ya hamasa ya Kitaifa ili kuhamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kujipangia utaratibu wa kwenda katika vituo vyetu vya afya ili kuchangia damu.

Lakini pia zoezi la uchangiaji damu ni kuendeleza kampeni ya kitaifa ya “Saidia Mama Mjamzito Ajifungue Salama”.

Washiriki

A. Viogozi wa serikali

1.Mh. Dr. Fenella E. Mukangara (MB) – Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo.
2.Mh. Mary Nagu (MB) Waziri wa Uwezeshaji na Uwekezaji
3.Mh. Amina Makilagi Mbunge na Katibu Mkuu wa Umoja Wa Wakina Mama Tanzania.
4.Mh. Meck Sadik Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
5.Mh. Anjela Kairuki- Mbunge. Makamu mwenyekiti kamati ya sheria ya bunge.
6.Mh. Jordan Rugimbana- DC Kinondoni.
7.Mh. Halima Mdee-Mbunge
8.Mh. Idd Azan – Mbunge
9.Mh. Abasi Mtemvu-Mbunge
10.Mh. Dr.Faustine Ndungulile-Mbunge
11.Mh. Magreth Sitta- MBunge na Mwenyekiti wa Kamati ya huduma ya jamii ya Bunge.
12. Stara Thomas - Balozi wa Mama na Mtoto

B.Taasisi na Makampuni.

1.Wawakilishi wa Vyombo Vya Ulinzi ( Jeshi la Polisi, JWTZ, JKT )
2. Wawakilishi wa Umoja wa Wanawake Tanzania, UWT.
3.Wawakilishi Chama Cha Madaktari Tanzania.
4.Wawakilishi MEWATA,
5.Wawakilishi NMB
6.Wawakilishi Tanzania Women Bank,
7.Wawakilishi Airtel,
8.Wawakilishi Diamond Trust Bank,
9.Wawakilishi NSSF,
10.Wawakilishi PSPF
11.Wawakilishi IPP Media, TBC1, Star TV, Mwananchi, Uhuru Publications etc.
12.Wawakilishi chama cha waandishi wa habari za michezo,Tanzania
13.Vijana,Wakina mama na Kina baba, Temeke, Kinondoni na Ilala.
14.Wanafunzi vyuo vikuu, Sekondari

C.Burudani.
Itatolewa na Msondo Music Band na Balozi wa Mama na Mtoto Stara Thomas.

D.Wito Kwa Wananchi.
Wananchi wote mnaombwa kuhudhuria kwa wingi kuja kuchangia damu ili kuokoa maisha ya kina mama wajawazito wanaohitaji damu.

E.Motisha.
Kwa yoyote atakaechangia damu kutakuwa na zawadi ya T-Shirt ya THPI na soda na atatambuliwa na damu salama kama mwanachama.

Ratiba

Na. Muda (Asubuhi) Tukio Mhusika
1. Saa 03:00-03:30 Kuwasili Wote

2. Saa 03:30-04:30 Kuwasili Mgeni Rasmi Mama Salma Kikwete, Mwenyekiti WAMA

3. Saa 04:30-05:00 Burudani Msondo Music Band

4. Saa 05:00- 05:10 Utambulisho na Utangulizi Katibu Mkuu THPI, Dr. Elisia Mpango

5. Saa 05:10-05:20 Ufafanuzi juu ya Kampeni ya Saidia Mama Mjamzito ajifungue salama Mratibu Taifa Mama na Mtoto THPI, Dr. Jubilate Msangi

6. Saa 05:20-05:30 Malengo ya Kuchangisha Damu Grace Maliva Mkurugenzi Masuala ya Damu - THPI

6. Saa 05:30-05:45 Hali halisi ya vifo vya kina mama wajawazito kitaifa na Duniani. Mkurugenzi Mtendaji THPI, Dr. Telesphory Kyaruzi

7. Saa 05:45-05:50 Burudani Stara Thomasi

8 Saa 05:50-06:10 Salaam kutoka Mkurugenzi Damu Salama Taifa Mkurugenzi Damu Salama

9 Saa 06:10-06:15 Salaam kutoka kwa viogozi mbalimbali Viongozi
Burudani Msondo Music Band

10 Saa 06:15-06:20 Salaam Kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh. Meck Sadic

12 Saa 06:30-06:35 Hotuba ya Mgeni Rasmi Mama Salma Kikwete- Mwenyekiti WAMA.

13 Saa 06:35-06:45 Shukrani Mwakilishi Chama Cha Wachangiaji Damu Tanzania

14 Saa 06:45-07:00 Burudani Msondo Music Band