Friday, April 6, 2012

THPI YAANZISHA KAMPENI YA KITAIFA YA KUCHANGIA DAMU ILIYOZINDULIWA NA MAMA SALMA KIKWETE


Mkurugenzi mtendaji wa THPI Dr. Telesphory Kyaruzi akitoa historia fupi ya taasisi hiyo pamoja na kuelezea kampeni ya "Saidia mama mjamzito ajifungue salama" kwa kuchangia damu katika awamu ya kwanza kitaifa. Wanaofuatilia kulia ni Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh. Dkt. Fenella E. Mukangara (MB), mgeni rasmi Mama Salma Kikwete mwenyekiti wa taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) , na katibu tawala mkoa wa Dar es Salaam Bi. Theresia Mbando.
Kampeni imelenga kukusanya damu kwa ajili ya kuwasaidia wakina mama wajawazito wanaohitaji damu kabla ya kujifungua wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua, na wale ambao wanajifungua kwa upasuaji.

No comments:

Post a Comment