Tuesday, May 15, 2012

WAHITIMU VYUO VIKUU TUMIENI TAALUMA YENU KUTENGENEZA AJIRA




Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Dk. Mary Nagu (MB) amewataka wahitimu wa vyuo vikuu katika fani mbalimbali hapa nchini kutumia elimu na utaalamu wanaoupata katika vyuo  mbalimbali hapa nchini  kwa kuweka mipango madhubuti ya kujiajiri.

Nagu aliyasema hayo wakati alipoongoza  matembezi ya “SAIDIA  MAMA MJAMZITO KUJIFUNGUA SALAMA” yaliyoandaliwa na Taasisi ya Madaktari wahitimu wa Vyuo Vikuu Tanzania (THPI) yaliyoanzia katika hospitali ya Manispaa ya Temeke mpaka Ofisi za Manisipaa ya hiyo, Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Februari 2012.

“Kwa niaba ya serikali napenda kuwapongeza Taasisi ya Madaktari Wahitimu wa Vyuo Vikuu Tanzania kwa kuwa chachu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika  kuwezesha vijana kujiajiri na napenda kuwahakikishia kuwa serikali inatambua mchango wenu wa kuunga mkono serikali katika kuboresha huduma za afya kwa akina mama na watoto” alisema Nagu

Aliongeza kuwa maendeleo ya elimu  nchini ya mechochea kuongezeka kwa vyuo vikuu hapa nchini na idadi ya wahitimu katika vyuo hivyo , ikiwa ni ishara ya uthubutu na utayari wa serikali katika kuwekeza na kusimamia sekta ya elimu hapa nchini lakini bado idadi ndogo ya wahitimu wanaoweza kupata ajira  katika sekta ya umma na binafsi kutokana na ufinyu wa nafasi hizo.

Aidha  Nagu alifafanua kuwa pamoja na kuwa Taasisi hiyo kuwa  inatengeneza ajira kwa vijana jambo kubwa  inalolitekeleza vizuri ni kwa kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha afya ya Mama mjamzito hapa nchini ,mpango wenye lengo la kupunguza  vifo kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga.

Awali akimkaribisha Nagu, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Madaktari Wahitimu Vyuo vikuu Tanzania,  Dk. Telesphory Kyaruzi alieleza kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni jinsi ya kuwapelekea huduma wanachi kwa wakati na kwa gharama wanazoweza kuzimudu.

Dr. Kyaruzi albainisha kuwa ukubwa wa changamoto huo pia unatokana na jinsi ya kuwafikia wananchi na hasa akina mama.

Katika mwaka 2010 kumekuwa na mafanikio makubwa katika kupungua kwa vifo vya mama wajawazito na wototo kufikia 454 kati ya watoto hai 100,000 kutoka 578 kwa mwaka 2005.



Friday, May 4, 2012

DKT. JAKAYA KIKWETE ATANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI



Mh. Dr. Fenella E. Mukangara (MB) (Katikati) atangazwa kuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

MAWAZIRI

1. OFISI YA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,

2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H.  Suluhu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

3.  OFISI  YA WAZIRI MKUU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

4.  WIZARA

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,
Waziri wa Ujenzi
Dr.  John P. Magufuli, Mb.,
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,
Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,
Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof.  Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof.  Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,
Waziri wa  Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,
Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,

Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,
Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,
Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,
Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,

5. NAIBU MAWAZIRI

OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI

6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

7.OFISI YA WAZIRI MKUU

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,

8. WIZARA MBALIMBALI

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,
Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,
Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,
Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
4 Mei, 2012